WORLD SOLUTION

WORLD SOLUTION
full

best news best news best temlates best templates best templates best news best news

Subscribe For Free Updates!

We'll not spam mate! We promise.


EDITING BADO ZINAENDELEA.-- USIACHE KUTEMBELEA BLOG YETU ANGALAU MARA 1 KWA SIKU HAKIKA UTAKUA WA TOFAUTI.-- ENDELEA KUFURAIA BLOG YETU.
#htmlcaption1 Go UP! Pure Javascript. No jQuery. No flash. #htmlcaption2 Stay Connected

Thursday, 18 July 2013

Mwakyembe- Si haki kulipa kuingia stendi Ubungo



 
·     
WAZIRI wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe amesema haoni msingi wa wasafiri kulipa kiingilio cha sh 200 kwenye Stendi kuu ya Mabasi yaendayo mkoani cha Ubungo (UBT).
Alisema jana hafurahii hali wanayokutana nayo wasafiri wanaotumia kituo hicho kutokana na kubomolewa vibanda vilivyokuwa vikiwasaidia kujihifadhi kwa lengo la ujenzi wa mradi wa mabasi yaendayo kasi.
Dk Mwakyembe ambaye ameahidi kukutana na wahusika kufanyia kazi suala hilo, alisema hayo jana Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi ambao pamoja na maswali mbalimbali, walitaka kufahamu msimamo wake kuhusu hali ya kituo hicho.
“Sifurahii suala hilo…ni changamoto kubwa kwangu lakini nitawasiliana na ofisi ya Waziri Mkuu ambao ndio wanaofuatilia utekelezaji wa mradi huo wa mabasi ya kasi,” alisema Dk. Mwakyembe na kusisitiza hali ilivyo kituoni hapo ni kero na hakuna haja ya kulipa ushuru huo.
Kwa sasa katika kituo hicho kikuu cha mabasi, wasafiri wamekuwa wakihangaika kupata sehemu ya kujihifadhi kutokana na kubomolewa kwa mabanda.
Kabla ya kituo hicho kubomolewa, uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam ulikuwa umesema Mei mwaka huu kituo hicho kingekuwa kimehamishiwa eneo la Mbezi Luis jambo ambalo hadi sasa halijatekelezwa.

Please Give Us Your 1 Minute In Sharing This Post!
SOCIALIZE IT →
FOLLOW US →
SHARE IT →
Powered By: BloggerYard.Com

1 comments: