Interpol yamtia mbaroni Alex Massawe Dubai

Alex Massawe
Kwa ufupi
Mkuu wa la Shirika la Polisi la Kimataifa
(Interpol), Tawi la Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Gustav
Babile aliliambia gazeti hili jana kwamba Massawe alikamatwa kati ya
Juni 20 na 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Dubai
akitokea Afrika Kusini.
Kwa nini Massawe anatafutwa
Aprili 4 mwaka huu, mfanyabiashara huyo alitajwa
mahakamani katika kesi ya mauaji ya mfanyabiashara Onesphory Kituly
ambaye aliuawa katika mazingira ya kutatanisha Novemba 6, 2011 akiwa
nyumbani kwake Magomeni, Dar es Salaam.
Katika kesi hiyo ambayo mshtakiwa wa kwanza ni
mfanyabiashara maarufu, Abubakar Marijani ‘Papaa Msofe’ na mshtakiwa
mwingine, Makongoro Joseph Nyerere alitoa malalamiko mbele ya Hakimu
Mkazi, Agnes Mchome baada ya Wakili wa Serikali, Mwanaisha Kombo kudai
upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kuomba tarehe mpya ya
kuitaja. Mshtakiwa huyo, aliomba jalada la kesi yao lipelekwe mahakamani
hapo kwa ajili ya kulifanyia kazi na kutuhumu kuwa ndugu wa marehemu
Kituly hawataki maendeleo ya kesi yao hadi Massawe akamatwe.
adobe photoshop cs6 serial
ReplyDelete